Pages

Ads 468x60px

LIKE THIS PAGE FIRST.

Saturday, September 28, 2013

MANENO YA AUNT EZEKIEL KUKANUSHA MANENO YA MTAANI......!!!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiNSczvn3VzvmNHB6F4NiCc8Wrg9HJErDv35NkH4BSLBSEd31HFxpuM-R2PuQodXfh9Tu9cq3Fs75AQyK2XVgjCrk2DZZl8wtYcTVRYjWt2awVsOgKbzxahCjVuBvH-5xh2yQEmKsky/s1600/Aunt+Ezekiel+(2).JPG
Stori: Mayasa Mariwata
STAA wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel amesema hana mkosi kama watu wasiomtakia mema wanavyoeneza maneno mitaani.

Akipiga stori na paparazi wa Ijumaa juzikati, Aunt alisema kuna baadhi ya watu wasioitakia mema ndoa yake wamekuwa wakieneza maneno kwamba ana mkosi ndiyo maana kila mwanaume anayekuwa naye hupatwa na balaa.
 
http://api.ning.com/files/WNymk69HNNMgiWP51IX94Gff9ntnip52E1X0ojLIqvdBO7JIcV1o7vU*HJEQkpyJ3gIv9SRxwzy9sOklaBsh22V2USTw8gbQ/aunthii.jpg?width=600 Staa huyo aliongeza kuwa haumizwi kichwa na maneno hayo kwa kuwa anaamini kila kinachotokea katika maisha yake ni mipango ya Mungu.
“Maneno yao ni imani potofu na siwezi kumfikiria mwanaume niliyewahi kuwa naye huko nyuma kabla ya kuolewa na mume wangu Demonte kwani hakuna baya lililomfika tangu tulipooana,” alisema Aunt.

No comments:

Post a Comment