Pages

Ads 468x60px

LIKE THIS PAGE FIRST.

Wednesday, July 24, 2013

MAN UNITED ITAFANIKIWA KUMNASA FABREGAS?



Cess Fabregas
Klabu ya Barcelona imeiambia Manchester United kuwa haina nia ya kumuuza nyota wake Cesc Fabregas.
Manchester United, imethibitisha kuwa iliwasilisha tena ombi la kumsajili mchezaji huyo kwa kitita cha pauni milioni thelathini, lakini ripoti zinasema kuwa ombi hilo limekataliwa.
Rais wa Barcelona Sandro Rossel, amekariri kuwa klabu hiyo haina nia ya kumuuza mchzaji huyo kwa klabu yoyote.
Kocha wa Manchester United, David Moyes amenukuliwa akisema huenda wasifanikiwe kumsajili mchezaji huyo.
Hata hivyo Moyes amekiri kuwa naibu mwenyekiti wa klabu hiyo Ed Woodward, angali anafanya kila juhudi ili kuhakikisha kuwa wamemsajili mchezaji huyo.
Mara ya kwanza United iliwasilisha ombi la kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka ishirini na sita kwa kitita cha pauni milioni ishirini na tano, lakini pendekezo hilo lilikataliwa na Barcelona.


David Moyes Kocha wa Manchester United
Siku mbili tu baada ya United kuwasilisha ombi hilo, Woodward alikatiza ziara yake nchini Australia na kurejea nyumbani kuongoza mikakati ya kumsajili Fabregas, kabla ya muda wa mwisho wa usajili kukamilika.
Barcelona haijatoa taarifa yoyote, lakini kuna habari kuwa huenda matatizo yanayokumba klabu hiyo kwa sasa yamechangia pakubwa uamuzi huo kukataliwa.
Kocha wa Barcelona Tito Vilanova alijiuzulu kutokana na matatizo ya kiafya.
Haijulikani ikiwa uamuzi wa Chelsea wa kutaka kumsajili mshambulizi wa Manchester United Wayne Rooney umechangia klabu hiyo kutaka kumsajili Fabregas

No comments:

Post a Comment