Pages

Ads 468x60px

LIKE THIS PAGE FIRST.

Sunday, December 29, 2013

BREAKING NEWS.......WIZARA YA FURSA YAFUNGUKA MBELE YA MKURUGENZI WA CLOUDS MEDIA GROUP.


  Kutoka kulia  ni  Bw. Riziki Shaweji (Waziri wa Fursa,Mipango na Uwezeshaji CBE-Dodoma),Bw.Ruge Mutahaba (Mkurugenzi Mtendaji  Clouds Media Group) na Bw. Alex Morio (Katibu Mkuu wizara Mipango na Uwezeshaji CBE-Dodoma).

 Wizara ya Fursa, Mipango na uwezeshaji wa serikali ya wanafunzi CBE jana tarehe 28/12/2013 imeondoka na kuelekea  Dar es Salaam kama sehemu ya kutekeleza majukumu yake.
Akizungumza na Wizara ya Habari,Waziri wa wizara hiyo Mhe, Riziki Shaweji ambaye ameambatana na katibu mkuu wa wizara hiyo Mhe. Alex Morio amesema leo (29/12/2013) wamekutana na Bw. Ruge Mutahaba mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group  kwa lengo la kupata ushauri na maoni mbalimbali juu ya fursa kwa vijana hususani kwa wasomi wa Elimu ya juu lakini pia kama wizara  kutoa mikakati iliyonayo  juu ya fursa kwa wasomi wa Elimu ya juu hususani Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Dodoma , hata hivyo wizara hiyo imepata fursa ya kuwasilisha Baadhi ya mikakati ikiwa ni pamoja na mkakati wa CBE kuwa na maadhimio ya ''CBE Day''  siku ambayo itaambatana na matukio mbalimbali, pia suala Maktaba kwa maana ya upatikanaji wa Vitabu chuoni,Suala la Mr. na Miss CBE, pamoja na hayo wamebainisha umuhimu wa uwepo wa fursa mbalimbali za kiuchumi kwa vijana wasomi katika mkoa wa Dodoma.
Bw.Ruge Mutahaba (Mkurugenzi Mtendaji  Clouds Media Group) akiwa katika moja ya  Semina ya  Fursa mkoani Tanga (October 2013)   

 Kwa upande wake Bw. Ruge Mutahaba amepongeza sana serikali ya wanafunzi wa CBE kwa kubuni na kuwa na Wizara ya Fursa, Mipango na uwezeshaji na kusema Mkoa wa Dodoma ni Mkoa wenye Fursa nyingi na wenye wasomi wengi wa Vyuo vya Elimu ya juu, na hivyo ni mhimu sana kwa Taasisi za Elimu ya juu kutumia Elimu yao  kwa kuwa wabunifu na kuchangamkia Fursa zilizopo ili kuleta chachu ya maendeleo katika jamii kwa ujumla.
Ikumbukwe kwamba Ruge Mutahaba amekuwa mstari wa mbele kupigania vijna katika nyanja za uchumi kwa maana ya kuibua fursa zilizopo katika Mikoa mbalimbali nchini Tanzania kwa lengo la kupambana na dhana ya ukosefu wa Ajira kwa vijana.
Kwa upande wake Waziri wa fursa, mipango na uwezeshaji Mhe; Riziki Shaweji "amepongeza hatua na mikakati pamoja na juhudi zinazoonyeshwa na Bw. Ruge Mutahaba kwa kuwa na nia ya dhati ya kuwakomboa vijana kwa lengo la  kupunguza suala la ukosefu wa ajira nchini" Waziri huyo ameongeza kwa kusema Wizara ya Fursa imejipanga kuibua na kufungua milango kwa wanafunzi wa chuo hicho kuchangamkia Fursa zilizopo Mkoani Dodoma ili kuleta chachu kwa wasomi wa vyuo vya Mkoa wa Dodoma na Tanzania kwa ujumla .
Kuna kila sababu ya wasomi kuunga mkono juhudi mbalimbali zinazoonyeshwa na wadau kama Ruge Mutahaba kwa maslahi ya Taifa kwa ujumla.

Bw. Riziki Shaweji (Waziri wa Fursa,Mipango na Uwezeshaji CBE-Dodoma)

  Bw. Alex Morio (Katibu mkuu  wa Fursa,Mipango na Uwezeshaji CBE-Dodoma) akiwasilisha  mikakati ya wizara yake kwa  Bw, Ruge Mutahaba (Mkurugenzi Mtendaji Clouds Media Group)

    Bw. Riziki Shaweji (Waziri wa Fursa,Mipango na Uwezeshaji CBE-Dodoma) akiwasilisha  mikakati ya wizara yake kwa  Bw, Ruge Mutahaba (Mkurugenzi Mtendaji Clouds Media Group)
                                                      Mhe; Remidus M. Emmanuel
                                                Rais wa Serikali ya Wanafunzi - CBE - Dodoma

Rais wa Serikali ya Wanafunzi Campus CBE - Dodoma Mhe; Remidus M. Emmanuel.Amepongeza  utendaji wa  wizara ya Fursa,Mipango  na Uwezeshaji  na kuongeza kuwa  umefika wakati  kwa wasomi  wa Taasisi za elimu ya juu  kuangalia namna bora ya kupunguza changamoto ya ajira nchini. "Tayari kama serikali ya wanafunzi tuko katika muendelezo wa kuchangamkia Fursa ya ufugaji nyuki katika Wilaya ya Chamwino kwa ushirikiano mkubwa wa mkuu wa Wilaya hiyo  Mhe.Fatma Ally.
"Inapendeza kama serikali ya wanafunzi inapokuwa mfano kwa wanafunzi hatua ambayo italeta mapokeo chanya kwa wanafunzi wote kwa  kuthubutu na kuchangamkia fursa kwa kuiga mfano wa viongozi wao"
Alisema Rais huyo na kusema  kuwa anaamini kila kitu kitawezekana kupitia wizara yake ya fursa, mipango na uwezeshaji, kwa kuchangamkia fursa zilizoko mkoani Dodoma kwa Maendeleo  ya CBE na Taifa zima  kwa ujumla .
Pia amepongeza juhudi zinazofanywa na  Bw. Ruge Mutahaba  kupitia kampuni yake ya Clouds Media Group na kuitaka jamii ya wasomi wa vyuo vyote nchini kumuunga mkono kwani juhudi zake zinalenga maslahi ya vijana wa Taifa zima la Tanzania.

No comments:

Post a Comment