MANENO YA OMMY DIMPOZ KUHUSU SHOW ZA BONGO TUNALIPWA VIZURI KULIKO SHOW ZA NJE.
Msanii
anayefanya vizuri kwenye anga la muziki Bongo, Faraji Nyembo ‘Ommy
Dimpoz’ amefunguka kuwa shoo wanazofanya wasanii hapa nyumbani zinalipa
zaidi kuliko zile za nje. Ommy
Dimpoz amesema kuwa, kulipwa mkwanja mdogo kwenye shoo hizo za mamtoni
inatokana na idadi ya watu wachache wanaoingia kwenye shoo tofauti na
Bongo ambako watu huwa nyomi. “Naweza
kusema hapa nyumbani tunalipwa pesa nyingi kuliko ile tunayopata
tunapofanya shoo nje, inategemea pia unaenda kufanya shoo wapi lakini
ukweli unabaki kuwa hapa Bongo tunalipwa vizuri,” alisema msanii huyo Ambaye
juzikati alidondoka kutoka Marekani kisha kushusha bonge la shoo ndani
ya Ukumbi wa Kimataifa wa Burudani wa Dar Live pale Mbagala Zakhem siku
ya Idd.
No comments:
Post a Comment